Friday, December 17, 2010

UEFA DRAW

Round of 16 draw
AS Roma v FC Shakhtar Donetsk
AC Milan v Tottenham Hotspur FC
Valencia CF v FC Schalke 04
FC Internazionale Milano v FC Bayern München
Olympique Lyonnais v Real Madrid CF
Arsenal FC v FC Barcelona
Olympique de Marseille v Manchester United FC
FC København v Chelsea FC

Bofya hapa UEFA kwa habari zaidi.

Monday, December 6, 2010

BIG UP MSECHUUUUUUU........

Tusker Project Fame ni shindamo maarufu sana la kuibua vipaji vya Muziki katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati. Kwa Mwaka 2010, shindano hilo ambalo huwa linafanyikia nchini Kenya limefikisha awamu ya Nne huku nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Sudan ya Kusini zikishiriki.

Kwa Mwaka huu 2010, Tanzania iliwakilishwa na mwanadada Aneth Kushaba:


Na kisha akawepo mwanadada mwingine Leah Muddy:


Wadada hao kwa bahati mbaya kura hazikutosha na wakatoka mapema tena kwa kupishana Wiki moja kupitia mtindo maarufu wa mchujo wa ndani ya shindano hilo "PROBATION WEEK."
Mwakilishi wa Tatu kutoka Tanzania akawa ni Peter Mshechu:


Wawakilishi wetu wote wametuwakilisha vizuri tu na wanastahili pongezi. Msechu yeye ameweza kuvuka safari hiyo ndefu ya ushindani na hatimaye akaingia Nusu fainali akiwa na washiriki wenzake Sita kutoka nchi mbalimbali.

Kutoka Kushoto ni Steven (Kenya), Gaelle (Rwanda), Davis (Uganda), Amelina (Kenya), Msechu (Tanzania) na Rachael (Uganda).

Baada ya mchujo huo hatimaye Gaelle na Rachael wakaondoka na Washiriki Wanne waliobaki wakaingia Fainali ambayo imeng'arisha nyota ya Mshiriki Davis wa Uganda aliyeibuka kidedea wa mashindano hayo kwa Mwaka 2010.

Peter Msechu ameshika nafasi ya Pili na kuipeperusha vyema bendera yetu ya Tanzania katika mashindano hayo. Ametuwakilisha na kutufikisha mahali ambapo hatujawahi kupafikia tokea mashindano hayo yameanzishwa ambapo kwa mara ya kwanza tuliwakilishwa na Mwanamuziki Nakaaya.

Hongera sana Msechu kwa mafanikio hayo. Karibu tena nyumbani uendeleze kipaji chako kwa yale yote uliyayopata ukiwa katika mashindano hayo. Ni imani yangu kuwa Wadau wa Muziki wa Afrika Mashariki wanasubiri ujio wako mpya baada ya kumalizika kwa mashindano hayo.

Sunday, December 5, 2010

IVORY COAST NAKO MMMMHHHH!!!

Ivory Coast ni nchi ambayo imeshawahi kuingia kwenye mapigano makali ya makundi mbalimbali ya Waasi kutokana na masuala ya kukamata madaraka ya nchi. Lakini hali hiyo ilionekana kama imetulia kwa muda kabla ya hofu iliyopo sasa inayotokana na matokeo ya uchaguzi uliofanyika hivi karibuni nchini humo.

Katika uchaguzi wa Rais, awali Tume huru ya uchaguzi ya nchini humo ilimtangaza mpinzani Alassane Ouattara kuwa ndiye mshindi kwa asilimia 54; katika hali hisiyotabirika, Baraza la Kikatiba lenyewe likasema hapana! Bali mshindi ni Laurent Gbagbo kwa asilimia 51!!

Sasa mkanganyiko huo umechukua sura mpya baada ya Wagombea hao wa Urais kila mmoja kwa wakati na katika mazingira yake amekula kiapo cha kuwa Rais wa nchi ya Ivory Coast!! Ni hali ambayo imewashtua wengi kiasi cha msuruhishi Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini Thabo Mbeki kwenda nchini humo kutafuta suluhu la mkanganyiko huo unaotishia kuzuka kwa mapigano.

Nikualike tu ubofye hapa IVORY COAST kuona kinachoendelea.

Wednesday, November 24, 2010

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI 2010 - 2015

MUHIMU:
 Wizara ya Maji imeunganishwa na Kilimo na hivyo itakuwa ni Wizara ya Kilimo na umwagiliaji. Hapa Kilimo kwanza kimeongezewa nguvu ili kuondokana na kilimo cha msimu.
 Kazi, ajira na Vijan; kitengo cha Vijana kimehamishiwa Michezo na Utamaduni.
 Uwezeshaji wa Wananchi (Baraza la Uwezeshaji) ilikuwa katika Wizara ya Fedha na sasa imebidi kuipunguzia Hazina mzigo huu na kuielekeza Ofisi ya Waziri Mkuu.
 Wizara ya Miundombinu imepunguzwa, imegawanywa na kuwa na Wizara ya Ujenzi (Barabara na Viwanja vya Ndege) pamoja na Wizara ya Uchukuzi (Reli, Bandari na Usafiri wa Majini).


BARAZA LA JIPYA LA MAWAZIRI Lililotangazwa November 24, 2010
1. Waziri wa nchi Ofisi ya Rais; Uhusino na Uratibu – Stepehn Wasira
2. Waziri wa nchi ofisi ya rais; Menejiment ya Utumisi wa umma – Hawa Ghasia
3. Waziri wa nchi makamu wa Rais; Muungano - Samia Suluhu Hassan
4. Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu; Mazingira - Therezia Luoga Kofisa
5. OWM; Sera Uratibu na bunge – William Lukuvi
6. OWM; Uwekezaji na Uwezeshaji – Maria Nagu
7. OWM; TAMISEMI - George Mkuchika
8. OWM; Naibu Waziri TAMISEMI – Agrey Mwanri
9. OWM; Naibu Waziri – Elimu – Khassim Majali
10. Waziri wa Fedha – Mustafa Mkulo
11. Naibu waziri wa Fedha – Gregory Teu
12. Naibu Waziri Fedha – Bereila Ame Silima
13. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi – Shamsi Vuai Nahodha
14. Naibu Waziri Mambo ya Ndani – Khamis Kagasheki
15. Waziri wa Katiba na Sheria – Celina Kombani
16. Waziri Mambo ya nje – Bernad Membe
17. Naibu Waziri Mambo ya Nje – Mahadhi Juma Mahadi
18. Waziri wa ulinzi na JKT – Dk. Hussein Ally Hassan Mwinyi
19. Waziri wa Mendeleo ya Mifugo- Mathayo David mathayo
20. Naibu waziri Maendeleo ya Mifugo – Benedict Ole Nangolo
21. Wizari ya Mawasilaino Sayansi, Tekonolojia, – Prof. Makame Mnyaa Mbalawa
22. Naibu Waziri Mawasilaino Sayansi, Teknolojia – Charles Kiwanga
23. Waziri Ardhi Nyumba na makazi – Prof Anna Tibaijuka
24. Naibu Waziri Ardhi Nyumba na makazi – Godluck Ole Medeye
25. Waziri wa mali Asili an Utalii – Ezeki el Maige
26. Waziri wa Nishati na Madini – William Ngeleja
27. Naibu waziri wa Nishati na Madini - Adam Malima
28. Waziri Ujenzi wa Barabara, Viwanja vya Ndege – John Pombe Mgufuli
29. Naibu Waziri wa Barabara, Viwanja vya Ndege – Harrison Mwakyembe
30. Waziri wa Uchukuzi – Bandari, Reli, Majini – Omary Nongwi
31. Naibu waziri Bandari, Reli, Majini – Athuman Mfutakamba
32. Waziri wa Viwanda na Biashara – Cyril Chami
33. Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara- Lazaro Nyalandu
34. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi – Shukuru Kawambwa
35. Naibu Waziri Elimu na Mafunzo ya Ufundi- Philipo Murugo
36. Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii – Hussein Haji Mpanda
37. Naibu waziri Afya na Ustawi wa jamii – Lucy Nkya
38. Waziri wa Kazi na Ajira – Gaudencia Kabaka
39. Naibu waziri kazi na Ajira -Makongoro Mahanga
40. Waziri maendeleo ya jamii Jinsia na Watoto – Sophia Simba
41. Naibu Waziri Ummy Ally Mwalimu
42. Waziri wa Elimu, Habari, vijana na Michezo – John Nchimbi
43. Naibu Waziri Elimu, Habari, vijana na Michezo – Fenela Mkangala
44. Waziri wa ushirikiano Afrika mashariki – Samuel Sitta
45. Naibu Waziri Dk Abdalah Juma Abdalah
46. Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika – Jumanne Maghembe
47. Naibu Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika – Christopher Chiza
48. Waziri wa maji – Mark Mwandosya
49. Naibu Waziri wa maji – Gerson Luende
50. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais; Utawala Bora - Mathias Chikawe

Thursday, November 11, 2010

KINYANG'ANYIRO CHA USPIKA CCM.....

Viwanja vya Bunge mjini Dodoma vimetawaliwa na Vazi la Kijani leo baada ya zaidi ya Wabunge 200 wa Chama cha Mapinduzi CCM kukusanyika pamoja kwa ajili ya uchaguzi wa Mgombea wa Uspika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Siku ya Alhamisi Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi ilikutana katika Makao Makuu ya Chama hicho na kuyachuja Majina ya Wagombea 15 waliokuwa wameomba ridhaa hiyo. Jukumu la Kamati hiyo lilikuwa ni kubakiza Majina Matatu tu na ndipo:

Mama ANNA MAKINDA.....

Mama Makinda akiomba kura kutoka kwa Mmoja wa wajumbe wa Mkutano wa Kamati ya Wabunge wa CCM.

Mama ANNA ABDALAH.....

Hapo Mama Abdalah mwenye Kijani akiomba kura kutoka kwa Mama Sophia Simba muda mfupi kabla kuanza kwa uchaguzi.

Na Mama KATE KAMBA....

Mama Kamba akiomba kura kutoka kwa Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda kabla ya kufanyika kwa uchaguzi.

Basi hao ndio Wagombea Watatu waliopita katika mchujo huo wa NEC. Wote watatu ni Wanawake. Kwa nini?

Katibu wa CCM Yusuf Makamba anasema kuwa ni mpango wa makusudi wa chama chao ukilenga kuchochea zaidi vuguvugu la harakati za kumkomboa Mwanamke. Wanaamini kwa kufanya hivyo, mgombea atakayepita basi atakiwakilisha chama vizuri katika kinyang'anyiro cha Uspika na hatimaye Bunge hilo kupata kiongozi wake mkuu ambaye ni Mwanamke.

Tangu Tanzania imepata uhuru haijawahi kuwa na kiongozi mkuu mwanamke katika mihili yake yote mitatu ya nchi. Na Makamba anasema wamedhamiria kuifuta rekodi hiyo nchini na hatimaye kuandika historia mpya kwa moja ya mihili mitatu ya Taifa kuongozwa na Mwanamke. Ni mpango mzuri kwa kweli unaolenga kumkweza Mwanamke MWENYE UWEZO WA KUONGOZA. Mpango huo utawezekana? Tusubiri tuone.

Rungu la Kamati ya Wabunge wa CCM limekaa pia na kupiga kura za maoni za kumchagua mgombea mmoja kati ya hao Watatu. Na baada ya uchaguzi huo, taarifa iliyotolewa na Katibu Mwenezi wa CCM Kepteni John Chiligati ni kuwa Mheshimiwa ANNA MAKINDA ndiye mgombea wa uspika wa Bunge la Kumi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.



Mama Makinda amepata kura 211 kati ya 241 zilizopigwa. Mama Abdalah amepata kura 14 wakati Mama Kamba amepata kura 15, huku kura Moja tu ikiharibika.

Je, enzi za 'zama za spidi na viwango ndio zimeisha?'


"...amani ya ndani ya Bunge ni kanuni...," ni kati ya kauli alizozitoa Mama Makinda kuhusiana na utendaji wake wa kazi bungeni endapo atapata nafasi ya kuiongoza taasisi hiyo. Anasema kila jambo lina taratibu zake na hivyo kila Mbunge anapaswa kuzielewa kwa umakini kanuni zinazoliongoza Bunge ili awe na mahusiano mazuri na kiti cha Spika na akimalizia, "....ni kama mpira wa Miguu, lazima ucheze kwa kufuata sheria...."



Furaha kama hiyo itadumu endapo Mama Makinda atashinda uchaguzi wa Spika. Katika kinyang'anyiro hicho anakumbana na Wakili MABERE MARANDO ambaye amepitishwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA. Wabunge kwa umoja wao wataamua wanamuhitaji nani kati ya hao Wawili ili awe Spika wao mpya.

Ikumbukwe kuwa, hili ni Bunge lililotokana na hamasa ya Siasa waliyonayo Watanzania kwa hivi sasa. Ni hamasa hiyo iliyopelekea Bunge la Kumi kuongeza Wabunge wa kambi ya Upinzani....kuongeza kundi la Vijana kutoka Vyama vyote....kuongeza kundi la Wasomi......na hata viongozi wa dini.

Spika ajae ni vyema akaliangalia ongezeko la makundi hayo na kujua namna ya kufanya nayo kazi kwa pamoja bila mikwaruzano ya hapa na pale hisiyo na msingi kwa maendeleo ya Mtanzania.

Kila la kheri Mama Anna Makinda.....

MWANZO MZURI WA UGENINI.....

Baada ya kuona hizi Picha zifuatazo nikapata fikra kuwa kumbe mwanzo mzuri wa kuwa ugenini ni pale unapopata mapokezi mazuri kutoka kwa wenyeji wako:


Mheshimiwa Freeman Mbowe akikaribishwa mjengoni na Mheshimiwa Anna Kirango.


Mheshimiwa Samwel Sitta akimkaribiwa mjengoni Mheshimiwa Lyatonga Mrema.

SAFARI YA KUWASILI MJENGONI HIYOOO.........



Wa Kwanza Kushoto ni Ezekiel Dibogo Wenje, mbunge mteule kwa tiketi ya CHADEMA katika jimbo la Nyamagana Mwanza....wa katikati (nyuma) ni Hyness Kiwia, mbunge mteule kwa tiketi ya CHADEMA katika jimbo la Ilemela Mwanza na wa kulia ni Felix Mkosamali (Mwanafunzi wa Mwaka wa Tatu SAUT) ambaye ni Mbunge mdogo kuliko wote (Miaka 24) toka NCCR Mageuzi katika jimbo la Muhambwe Kigoma.


Baadhi ya Wabunge wateule wakiwa wanasalimiana na aliyekuwa Spika wa Bunge la Tisa Mheshimiwa Samuel Sitta (wa Pili kutoka kulia).


Aliyekuwa kiongozi wa Kambi ya Upinzani Mheshimiwa Hamad Rashid (kushoto) akisalimiana na aliyekuwa Spika wa Bunge la Tisa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samuel Sitta. Wote wamezikosa nafasi hizo za awali katika Bunge la Kumi.


Mbunge mteule wa jimbo la Same Mashariki Kilimanjaro (CCM) Mheshimiwa Anne Kilango-Malecela akimpokea kwa furaha Mbunge mteule wa jimbo la Hai Kilimanjaro (CHADEMA) Mheshimiwa Freeman Mbowe.


Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Dokta Wilbroad Slaa akiwasili katika viwanja vya Bunge kwa ajili ya Mkutano wa ndani wa chama hicho kati ya viongozi na Wabunge wateule wa CHADEMA.


Moja kati ya Wabunge wateule waliowasili na kufurahiwa basi ni Mheshimiwa Agustino Lyatonga Mrema wa Vunjo Kilimanjaro. Hapo alikuwa akipokewa na Mheshimiwa Sitta. Ni kama wengi hawaamini kumuona kwa mara nyingine tena mjengoni.


Kila la kheri kwa wote waliochaguliwa kwa ridhaa ya Wananchi. Zoezi la usajili kwa Wabunge hao limekwishahitimishwa. Kuanzia Jumamosi hii wataanza kula viapo vyao kabla ya kuwa Wabunge rasmi.

Wednesday, November 10, 2010

KIVUMBI IDODOMYA


Ziliaanza Kampeni na hatimaye Uchaguzi Mkuu umefanyika....viongozi nao wamepatikana: Madiwani, Wabunge na Rais. Mhiumili wa Tatu wa Nchi ni Bunge ambalo nalo pia lina Uongozi wake chini ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Spika Samuel Sitta (Mwenye Suti ya Kijivu akisalimiana na Wageni wa Bunge) ndiye alikuwa Kiongozi wa Taasisi hiyo katika Bunge la Tisa....na sasa ni Bunge la Kumi lenye ongezeko la Vijana....ongezeko la Wapinzani pia.


Mmoja wa Maafisa wa Bunge akiwa amebeba na kuyaingiza bungeni Majoho ya Spika na Naibu wake. Ni nani atachukua dhamana ya kuliongoza Bunge hilo? Chama cha Mapinduzi CCM kimepata Wagombea Kumi na Tatu; Chaama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimepata Wagombea Watano.

CCM wameshafanya mchujo na kuwabakiza Watatu: ANNA ABDALAH, ANNA MAKINDA na KATE KAMBA; CHADEMA kupitia kwa Mwenyekiti wao Freeman Mbowe hawakuweka hadharani ni nani wamempendekeza kuwania nafasi hiyo lakini tayari taarifa za kuaminika kutoka ndani ya chama hicho zinasema kuwa ameteuliwa MABERE MARANDO. Vita ni Vita Muraa!!!!

Tuvute subira kwani uchaguzi ni Ijumaa.

Monday, August 23, 2010

J. K. NDANI YA MWANZA

Kipenga cha Kampeni za Wagombea wa nafasi za Urais, Ubunge na Udiwani katika mwaka huu wa uchagazi, ndivyo hivyo kimeshapulizwa. Chama tawala...Chama cha Mapinduzi CCM kupitia kwa Mgombea wake urais Jakaya Kikwete na mgombea mwenza wake Ghalib Bilal imeshazindua rasmi kampeni zake huko jijini Dar es Salaam.

Baada ya Dar es Salaam, mambo yakaamia jijini Mwanza katika wilaya za Misungwi, Kwimba, Nyamagana na hatimaye uwanja maarufu wa CCM Kirumba.

Watu wakajitokeza kwa wingi kuwashuhudia Wagombea hao wa CCM:


Msafara ukaongozwa na Vijana waendesha pikipiki ambao hapa kwa Mwanza wanajulikana kwa jina maarufu la BODABODA kutokana na huduma wanayoitoa ya kubeba abiria:


Wanafunzi nao walijitokeza kama wanavyoonekana hapo wakiwa wamejipanga kumlaki mgombea urais wa CCM na timu yake:


Vijana wa CCM nao wakajipanga vilivyo kufanikisha tukio la Kampeni za CCM ndani ya jiji la Mwanza katika dimba la CCM Kirumba:






Na kisha Wagombea Urais na Umakamu wa rais wa CCM wakaonekana:




Hatimaye Wagombea hao wakajinadi kwa Wananchi wa Mwanza, wakisifu jitihada mbalimbali ambazo zimefanywa na Serikali ya awamu ya Nne chini ya Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake Ali Shein. Maeneo yaliyotajwa ni pamoja na Michezo, Miundombinu, Elimu, Afya na huduma za nishati na Maji vijijini.

Maeneo waliyoahidi kuyafanyia kazi zaidi ni kuboresha miundombinu ya Safari za Vivuko, Mwanza - Sengerema kupitia Kamanga; Ujenzi wa Nyumba za Walimu kwa kutumia pesa za ndani badala ya kuwategemea Wafadhili, kuiongezea Pesa benki ya rasilimali ili iweze kutoa mikopo zaidi kwa Wanawake na Vijana waweze kujiajili.

Hayo ni machache kati ya mengi tu ambayo CCM imekusudia kuyafanya kupitia ilani yake ya uchaguzi ya Mwaka 2010. Kiu ni utekelezaji wa hayo yanayohubiriwa na wanasiasa kwani katika kipindi hiki sauti za Wanasiasa zitahubiri mengi tu.

Ni wajibu wako Mwananchi kuyasikiliza....kuyatafakari na kuona kama yanatekelezeka.....lakini cha muhimu zaidi ni kwa wewe kutothubutu hata chembe kupuuzia kushiriki katika zoezi la kupiga kura. Maamuzi yako ni muhimu sana kwa ustawi bora wa nchi hii.

Mungu ibariki Tanzania. Mungu ubariki uchaguzi wa 2010.

Friday, August 13, 2010

FOLENI NDANI YA MWANZA

Mipango Miji bado inatupiga chenga sana. Mimi nilidhani Wahandisi wetu wa Miji inayokuwa kwa kasi hapa nchini wanatakuwa wanajifunza kwa uzoefu wa jiji la Dar es Salaam jinsi linavyopata shida ya foleni!!!

Lakini ni tofauti kwani sikutarajia kuona jiji la Mwanza linaanza kuona shubiri ya foleni ikiwa bado ni mapema sana. Watendaji wa jiji hawakushtuka toka mapema? Matokeo yake mambo haya kwa Mwanza yameshaanza kuzoeleka sasa wakati ndiyo kwanza jiji linaanza kukua kwa kasi.

Poleni Mwanza. Tumeshachelewa. Sasa hivi mjini kutakuwa hakuendeki.

TUSEME NI USAFIRI KAFIRI AU!!!??

Hivi karibuni tu tumesikia huko wilayani Sengerema Wanafunzi wakizama na kupoteza maisha. Mkasa wenyewe ni kutokana na usafiri wa Mtumbwi waliokuwa wakiutumia kwenda shule kuingiwa maji na kisha kushindwa kuhimili uzito wa maji na abiria walokuwemo na matokeo yake Mtumbwi wa Mv School Boat kuzama, mwisho wa siku Wanafunzi 19 wakapoteza maisha.


Lakini maisha ya Watu wa visiwani ndivyo yalivyo kila siku. Usafiri wao ni wa Mitumbwi tu iwe ni kutoka visiwani ama kurudi visiwani. Hawana vifaa vya kujikinga na maafa pindi wanapokuwa safarini. Hawana hata vifaa vya kujiokoa pindi ajali inapotokea na ndiyo hata maana wakati wa msiba wa Wanafunzi hao, ni Nyavu haramu aina ya Makokoro zinazokatazwa kwenye uvuvi lakini ndizo zilizokuwa mwokozi wa kufanikisha zoezi la kuopoa Maiti za Wanafunzi. Kwa faida yako tu ni kuwa Makokoro ndiyo yaliyotumika kuzonasa Maiti mithili ya Samaki wanavuliwa!!!!!!

Licha ya ajali kama hizo kuwa zinatokea mara kwa mara lakini hakuna mabadiliko katika usalama wa safari kama hizo za kwenda katika visiwa vidogovidogo. Ukizama ni ujanja wako tu wa kupiga mbizi. Si unaona kama hao jamaa chini hapo wanapiga Safari katika maeneo yenye kina kirefu halafu hawana tahadhali yoyote!!!!

Lakini ukweli unabaki pale pale kuwa ajali ni ajali tu. Hata Nyani hufa tu siku Miti yote anayoirukia akitereza. Ila kwa nini tahadhali ziwepo jamani!!!!!?????

Friday, July 30, 2010

"KOLD DIRINKS HERE!!!!!!"


Kuna vitu vingine unaweza kuviona katika Dunia hii na ukastaajabu kweli!! Kwanza hilo jengo lenyewe lilivyo.....halafu vinywaji baridi vinapatikana humo ndani!!!! Ama kweli usifanye uamuzi wa kujua hiki bora ama la eti kwa kuangalia tu muonekano wa nje wa hicho kitu.

Saturday, June 26, 2010

KUMEKUCHAAAA......


Moja ya vitu ambavyo huwa napenda kuviona katika Dunia hii ni pale Jua linapokuwa linachomoza! Huwa napenda sana hiyo mandhari na wakati mwingine huwa inanifanya nitulie kuangalia hilo tukio zima, wakati huo huo napata nafasi nzuri ya kutafakari mambo mbalimbali.

KOMBE LA DUNIA


Hizo Antena zimenyooka kwa wingi sana katika paa za nyumba za Uswazi. Kombe la Dunia hapo linaonekana live bila chenga. Waswahili watundu sana jamani. Yaani TUBE LIGHT kuwa Antena!!!!!?????

Friday, June 11, 2010

HIFADHI YA SERENGETI YAONGEZWA UTAJIRI

Serengeti ni kati ya hifadhi za Taifa ambazo zinawavutia watalii mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi. Ni hifadhi ambayo ukipata nafasi ya kuitembea, basi nafsi yako itafurahi kwa kuona Wanyama weeeengi…


Swala wanaonekana kwa wingi sana…


Nyumbu nao vilevile…


Viboko wazee wa majini…


Hata Nyani nao wamo…


Hao ni baadhi tu. Lakini pia katika hifadhi hiyo, wapo Twiga, Pofu, Tembo, Chui, Mbuni, Pundamilia na wengine kedekede! Na hivi karibuni Hifadhi hiyo imeongezwa thamani……imeongezwa utajiri.

Mwezi wa Tano 2010, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alitua katika hifadhi hiyo…


Vikundi mbalimbali vya utamaduni wa Mtanzania vikamkaribisha yeye na wageni alioongozana nao siku hiyo…




Mengine hayakumstaajabisha yeye tu, bali hata aliokuwa nao pia walibaki duuuuuuuuu!


Umeshawahi kuona Viatu kama hivyo hapo! Katika mazingira ya kawaida lazima uvishangae……


Ni kati tu ya burudani za asili ya Mtanzania ambazo zilionyweshwa siku hiyo katika hifadhi ya Serengeti.

Si Rais Kikwete tu…..vyombo mbalimbali vya habari vilifunga safari mpaka kwenye hifadhi hiyo kushuhudia utajiri huo ambao umeongezwa Serengeti.

Waandishi kutoka nchini walikuwepo…


Wengine walitoka SABC (Afrika Kusini), AP, REUTERS na kwingineko…




Na hata Balozi wa Marekani nchini Bwana Alfonso alikuwepo kufuatilia tukio hilo. Ona sasa alivyokuwa amejiachia……


Jamani wote hao walikusanywa na tukio moja tu. Ni la kurejeshwa kwa Faru weusi watano kati ya 32 ambao wanaingia nchini wakitokea huko Afrika Kusini. Historia inasema Faru hao wana asili ya Afrika Mashariki.

Mwanzoni mwa miaka ya 1960, Faru hao walipungua nchini na Afrika Mashariki kwa ujumla kutokana na vitendo vya ujangiri. Wapo waliokuwa wanawawinda wanyama hao eti kwa kuwa Pembe zao zikisagwa zinatoa unga ambao ni dawa nzuri ya kuongeza nguvu za kiume!

Hali hiyo ilipelekea kuchukuliwa kwa Faru wachache waliokuwepo, kisha wakapelekwa Afrika Kusini……..wakahifadhiwa na wakazaliana huko…….na hatimaye baada ya miaka takribani 50 kizazi cha Faru hao kimerejea nchini……


Ndege ikatua salama katika ardhi ya Tanzania, kisha ikafunguliwa……


Faru hao inasemekana hawatachukua muda mrefu kuyazoea mazingira yao ya awali pamoja na vyakula vinavyopatikana Serengeti. Na kwa kuanzia wameletwa na vyakula vyao vya muda……


Hatimaye wakaanza kushushwa…


Ilikuwa ni vigumu kuwaona kwa kuwa walikuwa katika makasha maalum…..na ulinzi ulianza kuimarishwa hapo hapo katika kiwanja kidogo cha ndege cha Seronera…


Kisha wakapakizwa kwenye Magari……
kvumjnh


Na safari ya kuelekea katika hifadhi ya Serengeti ikaanza…..


Hapo awali nimesema hifadhi ya Serengeti ina wanyama wengi lakini kwa sasa imeongezwa utajiri. Sababu ni kuwa Faru ni kati ya Wanyama watano wanaopendwa sana na Watalii duniani.

Sababu ya ujangiri haiitishi tena Serikali kwani Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Shamsa Mwangunga anasema kuwa kwa sasa wamejipanga kutokana na mafunzo mbalimbali ambayo wamekuwa wanawapatia Askari wao.

Wananchi nao wanasema ushirikiano wa kuwalinda wanyama pori kwa sasa upo kwani angalau wananufaika na kuwepo kwa rasilimali hizo. Wanasema siku hizi wanaona sehemu ya mapato yanayopatikana yanatumika kuimarisha miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Nae Rais Kikwete anasema dhana ya ulinzi hisiwape tena hofu Watanzania. Kwa nini? Anasema Faru hao watakuwa wanalindwa kwa Saa 24! Na kikubwa zaidi watakuwa na ulinzi wa kipekee kama wanavyolindwa viongozi wa nchi. Kila Faru atakuwa na mlinzi wake katika hizo Saa 24.


Kufikia mwaka 2013/2014 Serikali inatarajia kuwa Faru hao 32 wanaokuja kwa mafungu mafungu, watakuwa wameingia nchini na kusambazwa katika hifadhi mbalimbali za Taifa.

Kazi kwetu Watanzania kuushabikia utalii wa ndani.