Wednesday, November 10, 2010

KIVUMBI IDODOMYA


Ziliaanza Kampeni na hatimaye Uchaguzi Mkuu umefanyika....viongozi nao wamepatikana: Madiwani, Wabunge na Rais. Mhiumili wa Tatu wa Nchi ni Bunge ambalo nalo pia lina Uongozi wake chini ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Spika Samuel Sitta (Mwenye Suti ya Kijivu akisalimiana na Wageni wa Bunge) ndiye alikuwa Kiongozi wa Taasisi hiyo katika Bunge la Tisa....na sasa ni Bunge la Kumi lenye ongezeko la Vijana....ongezeko la Wapinzani pia.


Mmoja wa Maafisa wa Bunge akiwa amebeba na kuyaingiza bungeni Majoho ya Spika na Naibu wake. Ni nani atachukua dhamana ya kuliongoza Bunge hilo? Chama cha Mapinduzi CCM kimepata Wagombea Kumi na Tatu; Chaama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimepata Wagombea Watano.

CCM wameshafanya mchujo na kuwabakiza Watatu: ANNA ABDALAH, ANNA MAKINDA na KATE KAMBA; CHADEMA kupitia kwa Mwenyekiti wao Freeman Mbowe hawakuweka hadharani ni nani wamempendekeza kuwania nafasi hiyo lakini tayari taarifa za kuaminika kutoka ndani ya chama hicho zinasema kuwa ameteuliwa MABERE MARANDO. Vita ni Vita Muraa!!!!

Tuvute subira kwani uchaguzi ni Ijumaa.

No comments:

Post a Comment