Friday, February 26, 2010

WATANZANIA TUNAIPENDA NCHI YETU KWELI JAMANI
Kuna wakati fulani Tanzania tulisikia habari ya kusisimua juu ya mwenendo wa Watanzania kuipenda sana Nchi yao. Hii ni kwa mujibu wa maoni ya utafiti uliofanywa na taasisi ya kimataifa ya utafiti ya Afro Barometer yenye makao makuu nchini Ghana na kuongozwa na Amanda Lea Robinson wa Chuo Kikuu cha Stanford, Marekani.

Nchi ya Tanzania imeweka rekodi ya aina yake barani Afrika kwa kuibuka nchi pekee yenye Wananchi wenye mapenzi makubwa kwa taifa lao kuliko jambo au mfumo wowote wa kitamaduni, kiuchumi au kijamii unaowagawa katika makundi mbalimbali na matabaka.

Na kwa mantiki hiyo kuna yale mapenzi ambayo wakati mwingine mpendaji anaonekana kama "mwehu" kwa wale wasioelewa kuwa mwenzao kapendezwa na nini mpaka kufikia hatua hiyo ya "uwehu."


Mapenzi ya nchi huwa yanaonyeshwa na wazalendo wa nchi kwa namna mbalimbali. Mfano kuna wale ambao Timu yao ya Taifa inapocheza tu utawaona wamejipaka rangi za Taifa usoni,wamevaa fulana za Timu yao,wanapita mitaani wanaimba ili hali tu wenzao wanaoiwakilisha nchi waone kuwa kuna kundi kubwa la wazalendo lipo nyuma yao kuwaunga mkono wawakilishi wao.
Ebu ona mtiririko ufuatao katika Picha.

TAIFA STARS UWANJANI INAPIGA DUA


KOCHA MKUU NA BENCHI LAKE WANAOMBA DUA PIA



Na kama nilivyolueleza hapo awali kuwa uvaaji wa sare zenye kuiwakilisha nchi hauishii kwa Wachezaji, Kocha Mkuu na benchi la ufundi kama tulivyoona katika Picha zilizopita. Uvaaji wa naman hiyo pia hufanywa na Washabiki....hiyo yote ni katika kuonyesha uzalendo kwa Timu yao ikizingatiwa ya kuwa Timu hiyo inaliwakilisha Taifa.

Uvaaji wa Nguo zenye Rangi ya Taifa uwa unaambatana na Ushangiliaji wa nguvu uwanjani. Lengo hapa likiwa ni kuwapanguvu zaidi Wachezaji wacheze kwa bidii kuwafurahisha washabiki huku wakati huo huo wakisaka ushindi kwa ajili ya kulitea sifa Taifa lao.

Na ikumbukwe kuwa Ushabiki haujalishi Timu imeshinda ama imefungwa. Ni kushangalia kwa kwenda mbele tu bila kuchoka. Tena ushangiliaji huwa unanoga zaidi unapowaona Viongozi wakubwa wa Serikali wamejumuika uwanjani wakishangilia kama walivyo washabiki wengine.

USHABIKI WA VIONGOZI UNAONGEZA MORALI ZAIDI


"SAFI VIJANA KAZENI BUTI ZAIDI"


Unajua kila Mtu akishiriki kwa nafasi yake kuiunga Mkono Timu ya Taifa, mwisho wa siku Vijana wanacheza kwa bidii kwa nia ya kupata ushindi. Ushindi ukipatikana sasa...........Ni shangwe ya aina yake bila kujali huyu ni nani wala yule ni nani. Ebu ona hapa......

WASHABIKI WAKIWA WAMEPANDWA NA MZUKA WA USHINDI



Jamani hamna raha kama ya ushindi. Ushindi hauji hivi hivi. Licha ya maandilizi ya kutosha ya Timu lakini Washabiki wana nafasi kubwa sana ya kufanya Timu icheze kwa kujituma. Siku zote tuonyeshe uzalendo ama mapenzi mema kwa Timu yetu ya Taifa,tujitokeze kwa wingi kila inapocheza, tuishangilie bila kuchoka na tukubali matokeo.

Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeshiriki kikamilifu kwa nafasi yetu kuonyesha mapenzi kwa Nchi yetu kupitia anga hizo za Michezo kwani kama nilivyosema hapo awali ni kuwa Mapenzi ya nchi huwa yanaonyeshwa na wazalendo wa nchi kwa namna mbalimbali. Mfano kuna wale ambao Timu yao ya Taifa inapocheza tu utawaona wamejipaka rangi za Taifa usoni,wamevaa fulana za Timu yao,wanapita mitaani wanaimba ili hali tu wenzao wanaoiwakilisha nchi waone kuwa kuna kundi kubwa la wazalendo lipo nyuma yao kuwaunga mkono wawakilishi wao.

NAIPENDA SANA TIMU YANGU YA TAIFA. NAIPENDA SANA NCHI YANGU. MUNGI IBARIKI TAIFA STARS. MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Thursday, February 25, 2010

MAJANGA KATIKA MUONEKANO

MJENGO NDANI YA HAITI

Hakuna Jamii hisiyokumbwa na majanga katika Sayari hii ya Tatu maarufu kama Dunia. Na inaeleweka wazi kuwa majanga hayo huleta hofu miongoni mwa wakazi wa eneo husika na hata kwa wale wanaoishi karibu na husika. Wakati mwingine hofu hiyo huwakumba hata wakazi wa mbali....na hiyo inatokana na ile hali ya uhusiano uliopo baina ya pande zote mbili.

Yanapotokea majanga kama hayo sasa (kama ulivyoona katika Picha za hapo juu), vyombo vya habari huwa vinatumia nafasi zao za kuhabarisha Wananchi. Habari hizo huwa zinatolewa kwa njia ya Maandishi lakini pia kuna njia ya Picha. Kwenye Picha kuna ule usemi usemao kuwa, "Picha inazungumza Maneno mengi zaidi ya Maandishi."

Na katika usemi huo, tunaambiwa kuwa ukubwa wa matukio ya majanga mbalimbali duniani huwa yanaelezewa katika Picha kwa kutumia Wanawake na Watoto. Na hata ukweli wa hayo yanayosemwa juu ya hizo Picha tunaweza yaona kwa mfano wa hivi karibuni katika tetemeko la huko Haiti......hebu Picha zifuatazo.




Na ukijaribu kufuatilia matukio ya majanga mengi utaona huo ushahidi wa matumizi ya Picha zaidi za Wanawake na Watoto katika kuelezea ukubwa wa tatizo. Na wakati mwingine pia Wazee wanatumika katika Picha za majanga kama hayo.

Wanawake na Watoto wanatumiaka zaidi kwa kuwa muenekano wao huwa unavuta umakini kwa watu wengine kutaka kujua hasa ni nini kimewasibu wahusika hao. Kama unavyojua, Wanawake na Watoto huwa wanatia huruma sana. Ukiwaona wametumika katika tukio fulani ni lazima utajikuta unapatwa na huruma juu yao.....na mwisho wa siku unashawishika kuwasaidia.

Ila kwa huo mfano wa Haiti,Picha ambayo imefunika kuliko zote na imevuta hisia za watu wengi duniani ni hii utakayoiona punde ambapo mtoto alidumu chini ya jengo kwa siku kadhaa, anafikiwa na kikosi cha uokoaji na anapotolewa tu, anashangilia kwa mikono yote miwili kujiona kwa mara nyingine tena anarudi kwenye mwanga akitokea kwenye giza la chini ya Vifusi vya majengo.

Kwa matumizi ya Picha kama hizo, mwisho wa siku ujumbe unakuwa umefika juu ya janga husika.