Friday, December 17, 2010

UEFA DRAW

Round of 16 draw
AS Roma v FC Shakhtar Donetsk
AC Milan v Tottenham Hotspur FC
Valencia CF v FC Schalke 04
FC Internazionale Milano v FC Bayern München
Olympique Lyonnais v Real Madrid CF
Arsenal FC v FC Barcelona
Olympique de Marseille v Manchester United FC
FC København v Chelsea FC

Bofya hapa UEFA kwa habari zaidi.

Monday, December 6, 2010

BIG UP MSECHUUUUUUU........

Tusker Project Fame ni shindamo maarufu sana la kuibua vipaji vya Muziki katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati. Kwa Mwaka 2010, shindano hilo ambalo huwa linafanyikia nchini Kenya limefikisha awamu ya Nne huku nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Sudan ya Kusini zikishiriki.

Kwa Mwaka huu 2010, Tanzania iliwakilishwa na mwanadada Aneth Kushaba:


Na kisha akawepo mwanadada mwingine Leah Muddy:


Wadada hao kwa bahati mbaya kura hazikutosha na wakatoka mapema tena kwa kupishana Wiki moja kupitia mtindo maarufu wa mchujo wa ndani ya shindano hilo "PROBATION WEEK."
Mwakilishi wa Tatu kutoka Tanzania akawa ni Peter Mshechu:


Wawakilishi wetu wote wametuwakilisha vizuri tu na wanastahili pongezi. Msechu yeye ameweza kuvuka safari hiyo ndefu ya ushindani na hatimaye akaingia Nusu fainali akiwa na washiriki wenzake Sita kutoka nchi mbalimbali.

Kutoka Kushoto ni Steven (Kenya), Gaelle (Rwanda), Davis (Uganda), Amelina (Kenya), Msechu (Tanzania) na Rachael (Uganda).

Baada ya mchujo huo hatimaye Gaelle na Rachael wakaondoka na Washiriki Wanne waliobaki wakaingia Fainali ambayo imeng'arisha nyota ya Mshiriki Davis wa Uganda aliyeibuka kidedea wa mashindano hayo kwa Mwaka 2010.

Peter Msechu ameshika nafasi ya Pili na kuipeperusha vyema bendera yetu ya Tanzania katika mashindano hayo. Ametuwakilisha na kutufikisha mahali ambapo hatujawahi kupafikia tokea mashindano hayo yameanzishwa ambapo kwa mara ya kwanza tuliwakilishwa na Mwanamuziki Nakaaya.

Hongera sana Msechu kwa mafanikio hayo. Karibu tena nyumbani uendeleze kipaji chako kwa yale yote uliyayopata ukiwa katika mashindano hayo. Ni imani yangu kuwa Wadau wa Muziki wa Afrika Mashariki wanasubiri ujio wako mpya baada ya kumalizika kwa mashindano hayo.

Sunday, December 5, 2010

IVORY COAST NAKO MMMMHHHH!!!

Ivory Coast ni nchi ambayo imeshawahi kuingia kwenye mapigano makali ya makundi mbalimbali ya Waasi kutokana na masuala ya kukamata madaraka ya nchi. Lakini hali hiyo ilionekana kama imetulia kwa muda kabla ya hofu iliyopo sasa inayotokana na matokeo ya uchaguzi uliofanyika hivi karibuni nchini humo.

Katika uchaguzi wa Rais, awali Tume huru ya uchaguzi ya nchini humo ilimtangaza mpinzani Alassane Ouattara kuwa ndiye mshindi kwa asilimia 54; katika hali hisiyotabirika, Baraza la Kikatiba lenyewe likasema hapana! Bali mshindi ni Laurent Gbagbo kwa asilimia 51!!

Sasa mkanganyiko huo umechukua sura mpya baada ya Wagombea hao wa Urais kila mmoja kwa wakati na katika mazingira yake amekula kiapo cha kuwa Rais wa nchi ya Ivory Coast!! Ni hali ambayo imewashtua wengi kiasi cha msuruhishi Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini Thabo Mbeki kwenda nchini humo kutafuta suluhu la mkanganyiko huo unaotishia kuzuka kwa mapigano.

Nikualike tu ubofye hapa IVORY COAST kuona kinachoendelea.