Sunday, December 5, 2010

IVORY COAST NAKO MMMMHHHH!!!

Ivory Coast ni nchi ambayo imeshawahi kuingia kwenye mapigano makali ya makundi mbalimbali ya Waasi kutokana na masuala ya kukamata madaraka ya nchi. Lakini hali hiyo ilionekana kama imetulia kwa muda kabla ya hofu iliyopo sasa inayotokana na matokeo ya uchaguzi uliofanyika hivi karibuni nchini humo.

Katika uchaguzi wa Rais, awali Tume huru ya uchaguzi ya nchini humo ilimtangaza mpinzani Alassane Ouattara kuwa ndiye mshindi kwa asilimia 54; katika hali hisiyotabirika, Baraza la Kikatiba lenyewe likasema hapana! Bali mshindi ni Laurent Gbagbo kwa asilimia 51!!

Sasa mkanganyiko huo umechukua sura mpya baada ya Wagombea hao wa Urais kila mmoja kwa wakati na katika mazingira yake amekula kiapo cha kuwa Rais wa nchi ya Ivory Coast!! Ni hali ambayo imewashtua wengi kiasi cha msuruhishi Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini Thabo Mbeki kwenda nchini humo kutafuta suluhu la mkanganyiko huo unaotishia kuzuka kwa mapigano.

Nikualike tu ubofye hapa IVORY COAST kuona kinachoendelea.

No comments:

Post a Comment